Posts

JINSI YA KUMLINDA MTOTO WAKO DHIDI YA UKATILI.

Image
JINSI YA KUMLINDA MTOTO WAKO DHIDI YA UKATILI. Hakuna mzazi ambaye anapenda mtoto wake afanyiwe ukatili,lakini katika dunia hii ambayo tunaishi matukio ya ukatili yamekithiri sana,na kwa bahati mbaya sana yanafanyika kwa watoto,je kama wazazi au jamii tunatakiwa tufanye nini kumlinda mtoto dhidi ya ukatili? FATILIA KWA UKARIBU WATU AMBAO WANAKUWA KARIBU NA MWANAO (MARAFIKI AU NDUGU). Jaribu kufatilia tabia za  watu wa karibu na mwanao,je tabia zao zinaweza kumuathiri mtoto wako kwa namna gani,je tabia zao zinaweza kupelekea tukio la ukatili kwa mtoto wako,na kama unaona kuna tabia au viashiria ambavyo sio vizuri kwa mwanao,mweke mwanao mbali na watu hao. FATILIA KWA UKARIBU MICHEZO AMBAYO MWANAO ANACHEZA. Mara nyingi mtoto hucheza michezo ambayo ameizoea au mchezo mpya,fatilia sana michezo anayocheza akiwa mwenyewe na akiwa na wenzake,katika michezo hiyo utagundua kitu au utajifunza kitu kutoka kwa mwanao kipi kinaendelea kwake.Lakini pia unaweza ukagundua hatari ambayo mwanao anaw...

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2016/2017 YAMETOKA

Image
MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2016 BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA) leo Januari 31, 2017 limetangaza matokeo ya Mtihani wa Kuhitimu Elimu ya Sekondari, Kidato cha Nne kwa mwaka 2016, mtihani ambao ulifanyika mwishoni mwa mwaka jana ambapo ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.44 ukilinganishwa na ule wa mwaka jana. Katika matokeo hayo, shule za Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam zimeonekana kung’ara zaidi kwa kushika nafasi za juu wakati huohuo shule 6 za Dar es Salaam zikishika nafasi 10 za mwisho katika matokeo hayo. SHULE ZILIZOINGIA 10 BORA KITAIFA: Feza Boys Sec School – Dar es Salaam St. Francis Girls Sec School -Mbeya Kaizirege Junior Sec School – Kagera Marian Gilrs Sec School – Pwani Marian Boys Sec School- Pwani St. Aloysius Girls Sec School – Pwani Shamsiye Boys Sec School – Dar es Salaam Anuarite Girls Sec School- Kilimanjaro Kifungilo Girls Sec School- Tanga Thomas More Machrina Sec School – Dar es Salaam SHULE ZA DAR ES SALAAM ZILIZOSHIK...

MGUNDUZI KUTOKA TANZANIA

Image
MPEMBA EFFECT “MAJI ya moto yaliyochemka yanaganda (kuwa barafu) haraka zaidi kabla ya maji ya baridi” . ERASTO UPANDE WA KUSHOTO AKIWA NA DR.OSBORNE Ni ugunduzi wa kisayansi wa Mtanzania usiotajwa kwenye Vitabuni, Shuleni wala Vyuoni mwetu hapa nchini, lakini ni gumzo la kitaaluma katika Vyuo na taasisi mbalimbali za elimu za Mataifa mbalimbali. Ni “Udhani” (Hypothesis) unaoumiza vichwa vya wanasayansi wa Dunia yote, kuanzia Ulaya Magharibi, Amerika mpaka Asia. Ugunduzi huu wa kisayansi unaeoelezea “sifa ya kipekee ya maji” ulifanywa na mwanafunzi wa kidato cha tatu wa Kitanzania katika shule ya sekondari Magamba, Lushoto, Mkoani Tanga, mwaka 1963. Jina la Mwanafunzi huyo ni Erasto Bartholomeo Mpemba, jina ambalo sifa hiyo ya maji (physical phenomenon) imepewa, yaani “Mpemba effect”. Erasto Batholomeo Mpemba, kama ilivyokuwa kwa wanasayansi wengine maarufu duniani, alifanikiwa kugundua sifa hii muhimu ya maji kama ajali tu (accidental discovery), kama ilivyokuwa kw...

WATU WALIOWAHI KUTEMBEA MWEZINI

Image
Neil Armstrong (1930 - 2012)  na  Edwin 'Buzz' Aldrin ( alizaliwa  1930) Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Armstrong ni maarufu sana kwa maneno yake baada ya kuwa mtu wa kwanza kuukanyaga Mwezi: "Hatua moja ndogo kwa mwanamume mmoja, hatua moja kubwa kwa binadamu." Buzz Aldrin alimfuata. Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Wakiwa kwenye Mwezi, Neil na Buzz waliweka bendera ya Marekani na kuacha bango lililokuwa na ujumbe, "Hapa, wanaume kutoka sayari ya Dunia walikanyaga Mwezi kwa mara ya kwanza Julai 1969, AD (Baada ya Kuzaliwa kwa Yesu). Tulifika sote hapa kwa amani kwa niaba ya binadamu wote." Charles 'Pete' Conrad (1930 - 1999) Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Apollo 12 ilipaa angani kukiwa na tufani na radi, hali iliyosababisha nguvu za umeme kuzimika muda mfupi baada yao kuruka angani. Conrad mwishowe alipoukanyaga Mwezi, alisema kwa sauti: "Whoopee! Bwana, hiyo huenda ilikuwa hatua ndogo kwa Neil, lakini kwangu imekuwa ku...