RAIS DOKT POMBE JOHN MAGUFULI
LEO NAKULETEA HISTORIA YA RAIS WETU DKT MAGUFULI NA WASIFU WAKE
Dk. John Pombe Joseph Magufuli, alizaliwa Oktoba 29, 1959 wilayani Chato – wakati huo ikiwa Mkoa wa Kagera (sasa Mkoa wa Geita).
Ana Shahada ya Uzamivu ya Kemia (2006 – 2009) kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Elimu
Dkt. John Pombe Joseph
Magufuli alipata elimu ya msingi katika shule ya msingi Chato kuanzia
mwaka 1967 hadi 1974. Pia alijiunga na elimu ya Sekondari katika shule ya
Seminari Katoke-Biharamulo na Lake Sekondari-Mwanza kati ya mwaka 1975 hadi
1978. Aidha, mwaka 1979 hadi 1981 aliendelea na masomo yake ya kidato cha tano
na sita katika Shule ya Sekondari Mkwawa Mkoani Iringa.
Mwaka 1991 – 1994,
alisoma Shahada ya Uzamili (Kemia) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na
baadaye Chuo Kikuu cha Salford nchini Uingereza.
Mwaka 1985 – 1988,
alisoma Shahada ya Kwanza ya Elimu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
akichukua masomo ya Kemia na Hisabati.
Mwaka 1981 – 1982,
alisoma diploma katika Chuo cha Mkwawa akichukua masomo ya Kemia na
Hisabati.
Mwaka 1979 – 1981,
alipata elimu ya juu ya sekondari katika Shule ya Sekondari Mkwawa,
Iringa.
Mwaka 1977 – 1978,
alisoma elimu ya sekondari katika Shule ya Sekondari Lake, Mwanza.
Mwaka 1975 – 1977,
alisoma Shule ya Msingi Katoke, Biharamulo mkoani Kagera.
Mwaka 1967 – 1974,
alisoma Shule ya Msingi, Chato.
Mafunzo
Machi 1984 – Juni 1984
alihudhuria mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Mpwapwa mkoani Dodoma.
Januari 1984 – Machi
1984 alikuwa JKT Makuyuni, Arusha.
Julai 1983 – Desemba
1983 alikuwa JKT Makutupora, Dodoma.
Kazi
Mwaka 1982 hadi 1983
alikuwa Mwalimu Shule ya Sekondari Sengerema akifundisha masomo ya Kemia na
Hisabati na mnamo mwaka 1989 hadi 1995 alikuwa Mkemia wa Chama cha
Ushirika cha Nyanza (Nyanza Cooperative Union Ltd) Mwanza.
Harakati zake za
kisiasa zilianza mwaka 1995 alipogombea kiti cha ubunge katika jimbo la Chato
na kuteuliwa kuwa Naibu Waziri katika Wizara ya Ujenzi. Mwaka 2000 Dkt.
Magufuli aligombea na kushinda kwa mara ya pili na kuteuliwa kuwa Waziri wa
Wizara ya Ujenzi.
Aidha, katika chaguzi
za mwaka 2005 na 2010, aliendelea kuwania kiti cha ubunge katika jimbo la Chato
na kushinda uchaguzi huo na kuteuliwa kuwa Waziri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi hadi mwaka 2008 alipohamishiwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,
ambayo aliiongoza hadi mwaka 2010. Mwaka 2010 alipochaguliwa tena kuwa mbunge
wa Chato aliteuliwa kuwa Waziri wa Ujenzi.
Comments
Post a Comment